Total Pageviews

Monday, April 14, 2014

MAMA SALMA KIKWETE AKIFUNGUA RASMI MAONYESHO YA WANAWAKE WAJASILIAMALI

Mama Salma kikwete akiangalia kazi nzuri iliofanywa na kina mama wajasiliamali .Ukisema wanawake wanaweza wakiwezeshwa  si jui utakuwa unamaanisha nini wanawake wakiamua wanaweza kama inavyoona mwenyewe katika maonyesho haya

Friday, April 11, 2014

MATITI YA WASICHANA 'YAPIGWAPASI KUWAKIMBIZA WANAUME NCHINI KAMEROON

    

Dunia na hasa bara la Afrika bado lina safari ndefu ya kuziondoa kama siyo kuzifuta kabisa mila potofu ambazo zinaonyesha dhahiri kudumaza na kufifisha harakati za mwanamke kujikomboa na kujiletea maendeleo.
Moja ya mila hiyo potofu ni ile inayoenziwa na jamii   nyingi nchini Cameroun na Afrika magharibi ambayo ipo pia nchini Uingereza na Marekani kwa waafrika kutoka eneo hilo ambao huyapiga pasi matiti ya wasichana kwa kuyagandamiza kwa mawe ya moto au mchi lengo likiwa kuondoa mvuto wa wasichana wasifukuziwe na wanaume  wakware.
Inasemekana kwa kiasi fulani  imepunguza vitendo vya ubakaji watoto ila kitendo hicho  kina athari kubwa kimwili na kisaikolojia
Mpenzi  msomaji wa safu  hebu fuatilia  kwa makini kisa hiki kinaonyesha jinsi  gani mtoto wa kike anavyodhalilishwa na kuumbuliwa utu wake
W akati Mick-Sophie Anne alipoanza kuonesha dalili za kuvunja ungo akiwa na umri wa miaka 10, mama yake alipagawa kwa hofu ya wanaume kuanza kummendea bintiye huyo mpendwa.
Suluhu aliyoiamini ni kuchukua jiwe lenye moto na kulishindilia kwa nguvu kwenye matiti ya bintiye katika jaribio la kutaka kukinyoosha kifua chake ili kuondoa mvuto kwa wanaume.Kila jua lilipotoweka na giza kutawala,aliingia katika  jiko lake dogo lisilo na mwanga tayari kwa kumfayia mtoto wake kitendo hicho cha ukatili.
Akiwa humo, Priscille Dissake anaonekana akiliweka motoni jiwe lenye ukubwa wa ngumi na kisha kulishindilia kwenye matiti ya bintiye Mick-Sophie kwa muda wa miezi miwili. Huku dada wa Dissake alionekana akisaidia kumshikilia sakafuni kwa nguvu,ili kuzuia binti huyo asitikisike wakati wakufanyiwa kitendo hicho.
Utafiti mpya wa serikali umeonesha kuwa vitendo vya ‘upigaji pasi matiti’, kama mila hiyo potofu na haribifu inavyojulikana vimeshuhudia kupungua kwa vitendo vya ubakaji na ngono kutoka kwa ndugu wa karibu kwa asilimia 50 tangu vilipofichuliwa kwa mara ya kwanza mwaka 2005 na Shirika la Ushirikiano wa Kiufundi la Ujerumani (GTZ).
Lakini pia kampeni ya kitaifa ya kujenga mwamko shuleni, makanisani na katika vyombo vya habari imeweza kuibua uelewa kuhusu athari za kimwili na kisaikolojia zinazosababishwa na kitendo hicho. Hata hivyo pamoja na kazi kubwa na nzuri iliyofanywa na wanaharakati, watoto wa kike wapato milioni 1.3 bado ni waathirika wa mila hiyo ya kinyama kwa mwanadamu.
Ni sababu gani hasa ya msingi inayofanya akina mama hao kuendekeza mila hiyo potofu?
Jibu ni kwamba Kina mama hao wanaendekeza kitendo hicho kujaribu kuwalinda binti zao dhidi ya ngono za mapema, mimba za utotoni na ubakaji ulikithiri na kuwauthi akina mama hao juu ya vitendo hivyo
Mick-Sophie alianza kukua matiti mapema sana na akawa na mvuto kwa wanaume hususani wakware ambao wamezoea kutengeneza kuku huku wakiwa na chumvi mkononi
 Nilitaka kuulinda utoto wake na kumlinda dhidi ya wanaume wakware,” alisema Dissake, 46, akizungumza katika jiko lile lile, ambalo alikuwa akilitumia kuchoma jiwe kwa ajili ya kuligandamiza katika mwili wa binti yake zaidi ya miaka 20 iliyopita.
"Nilimzaa Mick-sophie wakati nilipokuwa na umri wa miaka 14 tu lakini baba yake hakuwepo" Kwakweli kilikuwa kipindi kigumu mno kwangu na sikutaka kitu kama hicho kimtokee binti yangu wa pekee niliyempenda kama mboni ya jicho langu.
Hata hivyo, juhudi za Dissake za kutaka kumwepusha mwanae huyo na majaribu hayo hazikuzaa matunda.Katika hali ya kusikitisha na simanzi kubwa kwa maelezo yake mwenyewe na ya mama yake, Mick-sophie alibakwa akiwa na umri wa miaka 13 na mjomba wake.
Mwaka mmoja baadaye alianza kufanya mapenzi na mwanafunzi mwenzake na akiwa na umri wa miaka 16, alizaa mtoto wake wa kwanza. Mtoto huyo aliyezaliwa wiki sita kabla ya wakati,alifariki dunia saa chache baadaye
Ijapokuwa Cameroon ni nchi pekee, ambayo utafiti wa kina umefanyika kuhusu upigaji pasi matiti, makundi ya haki za binadamu yanaamini ni mila iliyoenea sana katika ukanda huo wa Afrika Magharibia.
Aidha wanaamini umeenea miongoni mwa watu kutoka ukanda huo waishio ng’ambo, ikiwamo katika nchi za magharibi zenye sheria kali za kuwalinda watoto.
“Sisi Waafrika tunasafiri na utamaduni wetu popote tuendako, hivyo nina uhakika haya yanatokea Uingereza na Marekani pia,” alisema Margaret Nyuydzewira, ambaye alizaliwa Bamenda kaskazini magharibi mwa Cameroon, ambako vitendo vya upigaji pasi matiti ni jambo la kawaida.

Nyuydzewira ameanzisha taasisi ijulikanayo CAWOGIDO, ambayo inaendesha kampeni dhidi ya upigaji pasi matiti nchini Uingereza, ambako Wacameroon 9,600 wanaishi kwa mujibu ya sensa ya mwisho mwaka 2011.
Anasema kuna kesi kadhaa za upigaji pasi matiti zilizoripotiwa katika miji ya Birmingham na London nchini humo kipindi cha miaka michache iliyopita, lakini idadi inaweza kuwa kubwa zaidi.
“Watu ndani ya jamii zinazoendekeza mila hii wanajua nini kinachotokea, lakini ukweli unafichwa na kufanyika majumbani.Nikama ukeketaji  unajua kinachofanyika lakini kamwe hutamuona yeyote akiufanya".anasema Inatokea nchini Nigeria, Burkina Faso, nchini Chad, nchini CAR (Jamhuri ya Afrika ya Kati) na nchi nyingine za eneo hilo
 Hukiita kitendo hiki kwa jina lingine kwa lugha zao za asili,” anasema. Upigaji pasi matiti ni mila mpya kwa kiasi chake kwani ilianza kupata umaarufu zaidi katika miaka ya 1930 wakati Wacameroon walipoanza kuhama maeneo yao ya vijijini kwenda mijini kusaka ajira, mtaalamu wa tabia na mfanyakazi wa misaada Flavien Ndonko alisema
“Katika majiji haya, kuna kiwango cha chini cha udhibiti wa kijamii na kimila kutokana na tamaduni tofauti kujichanganya kwa uhuru. Mara wasichana walipoanza kwenda shule na kupata fursa ya kuwa nje ya kaya zao na hivyo pia kupata fursa za kujihusisha na ngono za mapema,” anasema Ndonko, ambaye hufanyaia kazi GIZ.
“Wakati maji safi na mlo bora na huduma za afya zikimaanisha kukua mapema kwa matiti ya wasichana, na kuwafanya waonekane wakubwa kuliko walivyo.Wastani wa umri wa ukuaji wa titi kwa wasichana nchini Cameroon umeanguka kutoka miaka 13.5 hadi chini ya miaka 12 kipindi cha miaka 100 iliyopita
Wakati Cameroon likibakia kama taifa la kihafidhina ambako upataji mimba nje ya ndoa hulaaniwa vikali na utoaji mimba ukiharamishwa, kina mama hutumia upigaji pasi kama kitendo cha kuhakikisha binti zao hawapati mimba ana kuacha shule.
Utafiti uliofanyika nchini humo mwaka 2011 umeonesha kuwa asilimia 20 hadi 30 ya wasichana wa Cameroon huota mimba kabla ya kufikisha umri wa miaka 16 na thelathini moja huacha masomo yao.Takwimu hizo zinaweza kueleza mwelekeo usio wa kawaida wa kitendo hicho.

Utafiti mpya umeonesha kuwa asilimia 16 ya wasichana hasa katika eneo la Mbali Kaskazini ambako kuna utamaduni wa ndoa za utotoni –hujaribu kuyanyoosha matiti yao kwa mawe moto au  kwa kutumia mchi ili waweze kuchelewesha uvunjaji uongo wao na waendelee na shule.

Pamoja na kile Dissake na kina mama wengine wanachosema kuhusu lengo lao zuri kwa binti zao, bila kujua wanahatarisha kuwaacha binti zao kwa matatizo makubwa ya kimwili na kisaikolojia, wafanyakazi wa sekta za afya wanasema.

Utafiti wa serikali uliodhaminiwa na GIZ, ulionesha kuwa idadi kubwa ya waliohojiwa ilikuwa na matatizo tofauti tofauti ya kiafya ikiwamo saratani ya matiti.‘Tulibaini kuwa wasichana wenye umri wa miaka 20 waliokutwa na saratani ya matiti,” Ndonko alisema. “Hatujui kama kuna uhusiano wa moja kwa moja baina ya kitendo hicho na saratani, lakini inaibua wasiwasi huo.”
Asilimia 32 ya waliohojiwa walilalamikia maumivu katika matiti na asilimia 17 walizungumzia kuhusu majipu na vidonda. Asilimia 13 walieleza kuathirika na uzito wa matiti na asilimia nane walipata athari za kudumu za matiti kupinda, kwa mujibu wa utafiti.Athari za kudumu kimwili zinaweza kusababisha athari za muda mrefu za kisaikolojia pia, utafiti ulihitimisha
“Kwa kadiri wasichana wanavyokua na kukomaa, huwa wawezi kuonesha matiti yao kwa marafiki wa kiume na au waume zao,” Ndonko alisema. ‘baadhi ya wasichana hujihisi aibu kufanya ngono bila kuondoa nguo zao kutokana na kuficha matiti yao yenye kasoro.”
Lakini wote Ndonko na Nyuydzewira wanaamini kina mama hawapaswi kuchukuliwa hatua bali waelimishwe athari za kitendo hicho.“Tunapaswa kuwaelimisha kwanza na kuwaadhibu pale tu watakapoendelea na kitendo hicho,” alisema Nyuydzewira.“Tunapaswa kuwaelimisha kwanza na kuwaadhibu pale tu watakapoendelea na kitendo hicho,” alisema Nyuydzewira. 
Kuwaadhibu kina mama kunaweza kuwa kitu kigumu kwa sababu wasichana wengi wanaamini mama zao wako sahihi kwani wanawalinda.‘Inafaa kuanza na kina mama kwa sababu binti zao bado ni wadogo wanakubali kwa hofu au sababu ya heshima kwa wazazi wao,” alisema
Kuhusiana Dissake baada ya kuelimishwa alijihisi kuwa na hatia na kukiri kwamba alifanya kosa bila kujua akidhani anafanya kitendo cha busara.“Upigaji pasi matiti unaumiza sana kuliko uzaaji,” anasema Mick-Sophie Anne. Nimsamehe mama yangu, lakini kamwe sitasahau hili,” anasema.



Monday, March 31, 2014

MWANAMKE UKIAMUA UNAWEZA

    Mara nyingi ugumu wa maisha unaonekana kwamtu ambaye amekaa bila kujishughulisha,lakini maisha ni mepesi mno na siku zote naamini mwanamke anayejishugulisha lazima atafanikiwa.
    Kukatatamaa ni changamoto ambayo imekuwa ikiwakumba wanawake wengi,matokeo yake wanaishia kulalamikia ugumu wamaisha wakati hakuna wanachokifanya ili kuondokana na hali hiya.
     Kuwa jasiri na kutokatatamaa nisilaha tosha kwa mwanamke kufikia maendeleo ambayo wengi wamekuwa wakiyatamani.Uvivu na kutokujiamini ndio sababu inayowafanya wanawake kuendelea kuwa  tegemezi na kujiingiza katika biashara haramu.
    Siku zote kujiamini na kujipa moyo kwamba nitapambana kwa namna yeyote basi ujue lazima utashinda hatakama hautakuwa tajiri wa kupindukia walau kuweza kujimudu na kuweza kutunza familia.
Mwanamke akiamua anaweza
    Unapojishughulisha kamwe maisha hayawezi kukupiga chenga,hili ni jambo ambalo wamekuwa wakipambana nalo wanawake wengi hasa waumezao wanapofariki dunia,hujikuta wakilia marambili wakifikiria msiba na wakati huo huo wakifikiria ni jinsi gani ataitunza familia
      Mwaname ajiwekee misingi ya kuonyesha kuwa anaweza kusimamia na kuendesha familia hata kama mume wake akiaga dunia
     Wakati umefika sasa kwa wamawake kuacha kujifungia ndani  na kujiunga katika vikundi vya ujasiliamali ili kujikomboa kutoka katika wimbi la umasikini.
      Ni ngumu kwa mtu anaye kaa ndani halafu atarajie maendeleo,lazima utoke nje kujichanganya na wenzio hapo nidpo utakapokutana na mawazo ya aina tofauti yanayoweza kuwa chanzo cha maendeleo.

    Kuna kila sababu ya wasichana kuweza kujiwekea misingi tangu wakiwa wadogo kwa kuzingatia elimu ili kujikwamua katika wimbi la umasikini.
    Serikali pia kwa upande wake inapaswa kuwekeza zaidi katika elimu ya watoto wa kike ili kulifanya kundi hilo kuwa na mchango katika maendeleo ya taifa.
    Mwanamke akipewa elimu ya kutosha anaweza kuwa mchango mkubwa kwa jamii na taifa kwa ujumla,wanawake waliokosa elimu maisha yao yamekuwa yakuhangaika mno.
   Kuhusiana na tabia  ya wanaume kuwakataza wake zao  kujishughulisha  hilo ni tatizo kubwa ,mara nyingi hilo linatokana  na wanawake kuwa wabinafsi na kushindwa kuonyesha mafanikio wanayoyapata kwa waume zao.
   Kuna wanawake licha ya kuwa na mafanikio katika shughuli zao hawataki kushiriki katika maendeleo ya familia,hivyo kujikuata wakikumbana na changamoto kutoka kwa waume zao.
    Wapo ambao licha ya kujishughulisha hawataki kuchangia chochote katika familia,ndio maana baadhi ya wanaume hukasirika na kukataza wake zao kufanya biashara kutokana  na kutoona mafanikio.
    Mwanamke anayetoka anakilasababu ya kuonyesha tofauti na mtu asiye na shughuli,na hilo linatokana na namna ambavyo anajitoa na kushirikiana katika maendeleo ya familia na jamii kwa ujumla.

Thursday, March 27, 2014

Thamani ya mwanamke:Utangulizi

Habari msomaji wangu,karibu katika blogu yangu itayokuelimisha mambo mbalimbali kuhusu mwanamke wa Kiafrika.Lengo na dhumuni ni kuonyesha umuhimu na thamani ya mwanamke katika jamii.
Historia katika jamii ya makabila mengi nchini Tanzania na hata barani Afrika kwa ujumla mwanamke kwa miaka mingi alichukuliwa na kuonekana kama kiumbe dhaifu na kisicho na thamani yoyote ile ile katika jamii.

Hii inatokana na mila na desturi kumfanya mwanamke huyo kama chombo cha kumstarehesha mwanaume,kumzalisha na wengune walienda mbali zaidi kwa kumfanya kama mtumishi wa ndani au kijakazi.

Kama vile haitoshi wanawake hao pia walitumikishwa kama magunia ya kufanya mazoezi kwa vichapo,kashfa,udhalilishaji  unaotokana na mfumo duni na vitendo vingine vichafu ambavyo hapaswi kufanyiwa mwanamke na binadamu yeyote yule.

Lakini kadri siku zinavyokwenda mbele mwanamke thamani yake inasonga mbele katika maeneo mengi ya kisiasa,kiuchumi,utamaduni,mazingira na jamii kwa ujumla.

Wanawake hao kwa sasa hutumia fursa mbalimbali za kiuchumi na kijamii kamavile biashara, kilimo,ufugaji na shughuli nyingine nyingi ambazo wanawake wamekua msaada mkubwa si katika familia zao tu bali pia kwa Taifa kwa ujumla

Wapo wanawake ambao kiutendaji ,taaluma,umahiri na uaminifu wao umekua tegemeo kubwa kwa Taifa letu.Wanawake kwasasa wameshika nyadhifa nyingi serikalini,mashirika ya umma,sekta binafsi hadi ngazi za kimataifa.

Uzoefu u naonyesha mataifa mengi duniani yalio watumia wanawake yamepata ustawi mkubwa sana katika ujenzi wa uchumi wao.Hii inadhihirishwa na uwiano kati ya vijana wa kike na wakiume wanaojiunga katika shule za msingi na za sekondari na hata elimu ya juu.

Wanawake hao  sasa wamethubutu hata kusomesha watoto wao na wengine na wengine kuendesha familia zao.Mbali na msaada mkubwa katika kuendesha familia zao lakini pia msingi mkubwa wa malezi mazuri katika jamii hizo ulitokana na msimamo uliojengwa na wanawake hao.